Sudan: Chumba cha kuulia wapinzani wa Bashir chabainika, chabatizwa jina la White House

Publié le par Popote Ulipo Duniani

aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Wakati wakazi wa Sudan wakishughulika kama nyuki kuamua  iwapo Sudan Kusini itajitenga na Sudan Kaskazini na kujitawala kama taifa huru au la, kumebainika chumba  kilichokuwa kinatumika kusimangia na kuulia wapinzani wa Rais wa nchi hiyo , Omar El Bashir.

 

 

 

White House mpya


BBC iliripoti kuwa mwandishi wake amewahi kutinga chumbani humo ambamo umati mkubwa wa wapinzani wa Omar Bashir na wengine waliodaiwa kuwapa uungaji mkono wao wamekuwa wakisimangwa na  wakiuliwa kama nzi, wote  wakiwa ni kutoka Sudan Kusini

 

Chumba hicho kilichoko Juba,  jijini mwa Sudan kusini  , kimebatizwa jina sawa na lile la ikulu ya Jamhuri za Kimarekani, white House.

 

Mwandishi huyo wa BBC amesema kuwa kwa macho yake mwenyewe aliona mapingu yakining'inia paa la chumba hicho na  mabaki ya risasi sakafuni.


Idadi kamili ya watu waliopoteza maisha yao  ndani ya  White House haijajulikana, ila afisa mkuu mmoja  wa majeshi ya Sudan Kusini alkadiria kuwa watu hao wanafikia maelfu.

 

BBC Gahuza

 

Janvier Nshimyumukiza

 

 

Publié dans Habari muhimu

Pour être informé des derniers articles, inscrivez vous :
Commenter cet article