Sudan Kusini yajitangazia uhuru wake na kuwa taifa jipya kuzaliwa duniani

Publié le par Popote Ulipo Duniani

Sudan-Kusini.png

Sudan Kusini imejitenga na Kaskazini na kutangaza rasmi uhuru wake na kuwa taifa jipya kuzaliwa duniani.   

  

Nchi mpya ya Sudan Kusini ambayo Mji wake mkuu ni Juba,  itakuwa na utajiri wa mafuta lakini itakuwa moja ya nchi maskini kabisa duniani kutokana na mapigano yaliyoikumba kwa muda mrefu.  mapigano hayo yalipelekea watoto  kutopata nafasi ya kujifunza kiasi kwamba watoto chini ya miaka 13 hawasomi huku pia 84% ya wanawake hawajui kusoma na kuandika

 

Sehemu iliyopigwa rangi

nyekundu ndiyo Sudan Kusini

 

Ijapokuwa Sudan Kusin  imejitenga na kaskazini, Uraia ni  suala ambalo bado lipo na utata. Redio ya Taifa Sudan imeripoti kuwa uraia wa Wasudan Kusini wanaoishi kaskazini umekwishafutwa, na maelfu ya wafanyakazi Wasudani Kusini wanaofanya kazi kaskazini walilazamika kuacha kazi zao kabla ya kugawanyika.

 

Changamoto kubwa iliyopo ni kwamba Kaskazini na Kusini hazijaamua maeneo ya Abyei na Kordofan yenye utajiri wa mafuta yatachukuliwa na taifa gani.

 

Janvier Nshimyumukiza

 


 

 

 

 

Publié dans Habari muhimu

Pour être informé des derniers articles, inscrivez vous :
Commenter cet article